KAMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL) imesema imejipanga kuimarisha miundombinu ya mawasiliano na kwamba taasisi za umma zinazohamia mkoani Dodoma kutokana na amri ya Rais John Magufuli zisiwe na shaka, anaandika Pendo Omary.
Agizo la kutaka Serikali na Idara zake kuhamishia shughuli zake mkoani Dodoma kabla ya Septemba mwaka huu lilitolewa na Rais Magufuli 23 Julai mwaka huu na kusisitizwa tena na tena na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim.
Katika taarifa iliyotolewa leo jijini Dar es salaam na Nicodemas Mushi, Meneja Uhusiano (TTCL) amesema, “tupo tayari na tuna uwezo mkubwa wa rasilimali watu, vifaa na utaalam wa kutosha katika kutoa huduma za mawasiliano.
“Taasisi zote za umma zinazohamia Dodoma tunazishauri kutumia huduma za TCCL katika kufanikisha malengo yao ya kimawasiliano.”
Hata hivyo, zoezi la kuhamia Dodoma kabla ya Septemba mwaka huu limekosolewa na wanasiasa na wachambuzi wengi wa masuala ya kiuchumi kutokana na serikali kutojipanga vyema ikiwemo kutokuwa na bajeti wala miundombinu inayoweza kuhimili kuhamishiwa kwa serikali na idara zake zote kubwa mkoani humo.
More Stories
NMB yang’ara maonyesho ya Nanenane
Oman yavutiwa kuwekeza Tanzania
Waziri Madini: STAMICO imeingia kundi la wawekezaji