Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Trump atangaza kugombea urais uchaguzi wa 2024
Kimataifa

Trump atangaza kugombea urais uchaguzi wa 2024

Spread the love

 

WAKATI kura za uchaguzi wa bunge hazijamalizika kuhesabiwa, rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump ametangaza nia ya kugombea urais kwa mara nyingine kupitia chama cha Republikan katika uchaguzi wa 2024.

Hii itakuwa ni mara yake ya tatu kuwania, baada kumshinda mgombea wa Demokrat, Hilary Clinton mwaka 2016, na aliposhindwa kutetea kiti chake katika uchaguzi wa 2020. Inaripoti Mitandao ya kimataifa … (endelea).

Akiwa katika makazi yake ya Mar-a-Largo, Trump ametoa tangazo hilo huku wachambuzi wakiona ni kama kupuuzia madai ya Warepablikan kwamba ni yeye aliyechangia kukosekana kwa wapiga kura wengi.

Mpaka sasa bado analalamika kwamba uchaguzi uliopita alifanyiwa hila zilizomuwezesha rais wa sasa wa 46, Joe Biden kushinda.

Hata hivyo, anakabiliwa na hali ngumu ya kisiasa licha ya kwamba kasi yake inaonekana kutozingatia hilo.

Trump ametoa tangazo hilo jana tarehe 15 Novemba, 2022 akiwa na wasaidizi wake kisiasa pamoja na wafuasi wake katika makazi yake ya Mar-a-Largo yaliyopo katika jimbo la kusini la Florida, ambako amekuwa akiishi tangu alipoondoka madarakani mjini Washington, Januari mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!