Monday , 5 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Trump ampongeza Kigogo wa FBI
Kimataifa

Trump ampongeza Kigogo wa FBI

Spread the love

DONALD Trump, Rais wa Marekani amemwagia sifa James Comey, Mkurugenzi wa Shirika la Upelelezi (FBI) akidai ni mtu mahiri na amejipatia umaarufu kiasi cha kumzidi yeye, anaandika Wolfram Mwalongo.

Trump amesema hayo katika tafrija iliyoandaliwa Ikulu ya nchi hiyo iliyohudhuriwa na vigogo wa vyombo vya usalama vya ndani ya taifa hilo.

Hatua hiyo imechukuliwa kama njia ya kurejesha na kumaliza tofauti baina ya rais huyo na shirika hilo ambapo awali lilitoa taarifa za uchunguzi zikishutumu kuwa ushindi wa Trump ulisaidiwa kwa namna mbalimbali na Vladimir Putin, Rais wa Urusi.

Hata hivyo Rais Trump alikana madai hayo kwamba hayana ukweli wowote hivyo yanapaswa kupuuzwa na Wamarekani.

Barrack Obama, rais aliyemaliza muda wake alitilia mkazo na FBI kufanya uchunguzi zaidi na hatimaye taarifa zilithibitisha kwamba Urusi ilihusika katika udukuzi wa kompyuta za Chama cha Democratic ingawa Rais Putini wa Urusi alikanusha madai hayo.

Kwa sasa, mataifa hayo hasimu yanaonekana kupunguza uhasama hasa kutokana na uhusiano mzuri baina ya Putin na Trump.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Miili ya waliofariki kwenye ajali ya treni India, kukabidhiwa baada ya vipimo vya DNA

Spread the love  TAKRIBANI watu 260 wamefariki na wengine karibu 650 wamejeruhiwa...

Kimataifa

Kauli ya Rais wa China kuhusu ajira yawakatisha tamaa vijana

Spread the love  KAULI ya hivi karibuni ya Rais wa China, Xi...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Jeshi la Sudan lasitisha mazungumzo na wanamgambo wa RSF

Spread the love  JESHI rasmi la serikali ya Sudan, limesitisha ushiriki wake...

Kimataifa

Wakimbizi laki mbili wa Kongo, Burundi kuhemea chakula

Spread the love  SHIRIKA la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP), limetangaza...

error: Content is protected !!