Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Trump aitunishia misuli Iran, yajibu mapigo
Kimataifa

Trump aitunishia misuli Iran, yajibu mapigo

Donald Trump
Spread the love

BAADA ya Rais wa Marekani Donald Trump mwanzoni mwa mwezi Mei 2018, kujitoa katika mkataba wa kimataifa wa nyuklia na Iran wa mwaka 2015, ametangaza kuliwekea vikwazo vya kihistoria taifa hilo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Rais Trump jana tarehe 2 Novemba 2018 kupitia akaunti yake ya Twitter aliandika kwamba vikwazo vinakuja, huku taarifa ya Ikulu ya White House ikieleza kuwa, vikwazo hivyo pia vitalenga mataifa yanayoshirikiana na Irani katika masuala ya biashara.

Hata hivyo, taarifa hiyo ya Ikulu ya White House, inaeleza kuwa vikwazo hivyo havitahusu mataifa nane ambayo haikutaja jina, yanayofanya biashara na Irani, hasa uingizaji wa mafuta kutoka katika nchi hiyo.

Vikwazo vipya na vya zamani vya Marekani dhidi Iran, vinatarajiwa kuanza kutekelezwa Jumatatu ya Novemba 5 2018, ambapo vitaelekezwa katika sekta ya usafirishaji wa majini, taasisi za kifedha na biashara ya mafuta.

Katibu wa Hazina wa Marekani, Steven Mnuchin, aliongeza kuwa Iran itaondolewa na au kutengwa kwenye mfumo wa kifedha wa kimataifa, ikiwa ni pamoja na mtandao wa malipo wa kimataifa wa Swifti kutoka mjini Brussels nchini Ubelgiji, kusitisha huduma kwa taasisi za kifedha kutoka Irani, kitendo kitakachoathiri mfumo wa kifedha wa kimataifa wa taifa hilo.

Kufuatia mzozo huo, Umoja wa Ulaya (E.U) umearifu kwamba utalinda mataifa yake yanayofanya biashara halali na Iran.

Katika taarifa yao ya pamoja, mkuu wa masuala ya kigeni wa E.U, Federica Mogherine na mawaziri wa masuala ya kigeni kutoka nchi za Uingereza, Ujerumani na Ufaransa wamesema watalinda uchumi wa wa Ulaya hasa wa nchi zinazofanya biashara na Irani kwa mujibu wa sheria ya E.U na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

 Iran yajibu mapigo kupitia msemaji wa wizara ya mambo ya nje, Bahram Qasemi alinukuliwa na kituo cha luninga cha taifa hilo, akisema kuwa Iran ina ujuzi na uwezo wa kusimamia vyema masuala yake ya kiuchumi, na kwamba hakuna uwezekano wa Marekani kufanikisha matakwa yake ya kisiasa kupitia vikwazo hivyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Rais Tshisekedi amteua kiongozi wa wanamgambo kuwa Waziri wa Ulinzi

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi,...

Kimataifa

Raila Odinga: Tutafanya maandamano makubwa mara mbili kwa wiki

Spread the love KIONGOZI wa upinzani nchini Kenya, Raila Amollo Odinga ametangaza...

Kimataifa

Magharibi kuwekeza silaha Indo-Pacific, China yachochea

Spread the love KUVUNJIKA ushirhikiano wa China na Magharibi uliodumu kwa takribani...

Kimataifa

Ruto amlaumu Odinga kujaribu kuanzisha mgogoro kwa mara ya pili

Spread the love  RAIS wa Kenya William Ruto amesema kwamba hatakubali “kutoijali...

error: Content is protected !!