Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Trilioni nane zahudumia deni la Taifa
Habari za Siasa

Trilioni nane zahudumia deni la Taifa

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imesema hadi kufikia Aprili 2022, imetumia kiasi cha Sh. 8.0 trilioni, kati ya Sh. 10.6 trilioni, ilizopanga kugharamia deni la taifa na huduma nyinginezo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa hiyo imewasilishwa leo Jumanne, tarehe 7 Juni 2022 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha wa 2022/23, bungeni jijini Dodoma.

Katika hatua nyingine, Dk. Mwigulu amesema, hadi kufikia Aprili, 2022 jumla ya Sh. 29.40 trilioni zimetolewa kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa mpango na bajeti ya Serikali, kati ya fedha hizo, Sh. 10.61 trilioni zimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati Sh. 7.27 zikitolewa kwa ajili ya kuhudumia deni la Serikali, huku Sh. 6.73 zikitolewa kwa ajili ya mishahara na Sh. 4.79 kwa ajili ya matumizi mengineyo.

“Wizara imeendelea kusimamia deni la Serikali kwa mujibu wa Sheria, wizara imelipa deni lote lililoiva katika kipindi hicho la jumla ya Sh. 6.81 trilioni. Kati ya kiasi hicho, deni la ndani ni Sh. 4.21 trilioni. Aidha, deni la nje ni Sh. 2.60 trilioni, ikijumuisha riba ya Sh. 0.572 trilioni na mtaji Sh. 2.49 trilioni,” amesema Dk. Mwigulu.

Wakati huo huo, Dk. Mwigulu amesema wizara yake imefanya tathmini ya uhimilivu wa deni la Serikali kwa miaka 20 ijayo (2021/2022 hadi 2040/41), ambapo matokeo yake yanaonesha kuwa thamani ya sasa ya deni la Serikali kwa pato la Taifa ni asilimia 31.8, ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 55.

Dk. Mwigulu amesema, hadi Aprili 2022, ukusanyaji wa mapato ya Serikali umefikia Sh. trilioni 19.99, sawa na 93.3% ya makadirio ya kukusanya Sh. trilioni 21.42 , katika kipindi hicho. Kati ya kiasi hicho, mapato ya kodi yamefikia Sh. trilioni 17.20, sawa na 94.5% ya lengo la kukusanya Sh. trilioni 18.2.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!