JUMLA ya Sh milioni 250 zilizopatikana kutokana na tozo za miamala ya simu zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa Kituo cha Afya Rukuba kilichopo Musoma vijijini mkoani Mara. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).
Hayo yameelezwa na Mbunge wa Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo (CCM) alipotembelea ujenzi wa kituo hicho jana tarehe 4 Machi, 2022.
Aidha, baadhi ya wakazi wa Rukuba wameelezea furaha yao kutokana na ujenzi wa Kituo hicho na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha huduma za kijamii nchini.
Pamoja na mambo mengine Kituo hicho cha afya, kitakuwa na maabara ambayo jengo lake limekamilika, wodi ya mama na watoto ambayo ujenzi wake upo ngazi ya msingi na jengo la kituo kizima ambalo lipo ngazi ya kukaribia kuezekwa.
Leave a comment