Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko TLS yaendesha kongamano kukusanya maoni kuboresha haki jinai
Habari Mchanganyiko

TLS yaendesha kongamano kukusanya maoni kuboresha haki jinai

Spread the love

 

CHAMA cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), limeendesha kongamano la wazi la kukusanya maoni ya wadau juu ya namna ya kuboresha taasisi ya haki jinai nchini. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kongamano Hilo limefanyika leo tarehe 11 Machi 2023, katika makao makuu ya TLS, jijini Dar es Salaam na kuongozwa na aliyekuwa Rais wa chama hicho, Fatma Karume.

Akifungua kongamano hilo, Makamu Mwenyekiti wa TLS, Gloria Kalabamu amesema maoni yatakayokusanywa yatapelekwa katika kikosi kazi kilichoundwa na Rais Samia Suluhu Hassan, kuangalia namna ya kuboresha mfumo na taasisi za haki jinai.

“Hivi karibuni Dk. Samja ameunda tume kuangalia namna ya kuboresha taasisi haki jinai nchini, imeabza kazi na inakusanya maoni kwa sasa ambayo yatawezesha maboresho ya taasiai ya haki jinai,” amesema Kalabamu na kuongeza:

“TLS kama mdau wa sheria tumekuwa tukifanya makongamano mbalimbali kwa ajili ya kukusanya maoni kusudi tupate maoni ya watu mbalimbali, tumeona ni vyema wadau muhimu tukakusanyika tuangalie namna ya kushauri Serikali kufanya mfumo wa haki jinai inakuwa bora.”

Mbali na Karume, waongoza mdahalo huo ni Wakili Mwandamizi, Mpare Mpoki na aliyekuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM), Beatus Malima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!