Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TLS yaendesha kongamano kukusanya maoni kuboresha haki jinai
Habari Mchanganyiko

TLS yaendesha kongamano kukusanya maoni kuboresha haki jinai

Spread the love

 

CHAMA cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), limeendesha kongamano la wazi la kukusanya maoni ya wadau juu ya namna ya kuboresha taasisi ya haki jinai nchini. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kongamano Hilo limefanyika leo tarehe 11 Machi 2023, katika makao makuu ya TLS, jijini Dar es Salaam na kuongozwa na aliyekuwa Rais wa chama hicho, Fatma Karume.

Akifungua kongamano hilo, Makamu Mwenyekiti wa TLS, Gloria Kalabamu amesema maoni yatakayokusanywa yatapelekwa katika kikosi kazi kilichoundwa na Rais Samia Suluhu Hassan, kuangalia namna ya kuboresha mfumo na taasisi za haki jinai.

“Hivi karibuni Dk. Samja ameunda tume kuangalia namna ya kuboresha taasisi haki jinai nchini, imeabza kazi na inakusanya maoni kwa sasa ambayo yatawezesha maboresho ya taasiai ya haki jinai,” amesema Kalabamu na kuongeza:

“TLS kama mdau wa sheria tumekuwa tukifanya makongamano mbalimbali kwa ajili ya kukusanya maoni kusudi tupate maoni ya watu mbalimbali, tumeona ni vyema wadau muhimu tukakusanyika tuangalie namna ya kushauri Serikali kufanya mfumo wa haki jinai inakuwa bora.”

Mbali na Karume, waongoza mdahalo huo ni Wakili Mwandamizi, Mpare Mpoki na aliyekuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM), Beatus Malima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

error: Content is protected !!