UCHAGUZI wa Meya wa Jijini la Dar es Salaam umegeuka kitendawili baada ya Kaimu Mkurugenzi wa Jiji kuahirisha kwa mara ya nne, anaandika Happyness Lidwino.
Kumekuwepo na sintofahamu ya kupatikana kwa Meya wa Jiji kutokana na mvutano uliopo kati ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam ulipangwa kufanyika leo lakini kutokana na kuendelea kwa mvutano kuhusu washiriki walio na sifa ya kushiriki upigaji kura kwenye uchaguzi huo kutopatiwa ufumbuzi, mgogoro huo umeendelea kutokea.
Taarifa zaidi kuhusu kinachoendelea zitakujia hivi punde.
More Stories
Maandalizi Sensa yafikia asilimia 87 zikiwa zimebaki siku 48
Mahakama yasema uamuzi kesi ya kina Mdee haujakamilika
Mbivu, mbichi kesi ya kina Mdee kujulikana leo