Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Tiketi elfu 11 zimeshauzwa mchezo Simba na Yanga
Michezo

Tiketi elfu 11 zimeshauzwa mchezo Simba na Yanga

Spread the love

 

JUMLA ya tiketi elfu 11 zimeshauzwa kuelekea mchezo wa fainali wa Kombe la Shirikisho (FA) kati ya Simba dhidi ya Yanga utakaopigwa kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Kigoma … (endelea).

Mchezo huo utapigwa siku ya Jumapili, tarehe 25 Julai 2021, kuanzia majira saa 10 jioni.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, mkoani Kigoma, Meneja Biashara wa kampuni ya N-Card ambao wakatishaji tiketi kwenye mchezo huo wa fainali, Jackson Jaka amesema kuwa mpaka sasa zoezi hilo linaenda vizuri bila changamoto yoyote.

“Zoezi linaendelea vizuri hakuna tatizo lolote lilojitokeza mpaka sasa na huduma bado zinaendelea,” alisema Meneja huyo.

Meneja huyo aliongezea kuwa wameweka vituo 11 kwa ajili ya kufanya mauzo hayo kwenye mji wa Kigoma, huku kati ya vituo hivyo, saba ni magari yanayotembea maeneo mbalimbali na vituo vinne ni rasmi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!