Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Michezo ‘Tik Tak’ kuimaliza Plateau mbele ya Simba
Michezo

‘Tik Tak’ kuimaliza Plateau mbele ya Simba

Haji Manara
Spread the love

‘TIKI Taka mpaka kwa Mkapa,’ ndio kauli mbiu wanayoingia nayo klabu ya Simba kwenye mchezo wa marudiano wa klabu bingwa barani Afrika hatua ya awali dhidi ya Plateau kutoka nchini Nigeria. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam …  (endelea).

Mchezo wa mzunguko wa kwanza ulichezwa kwenye mji wa Jos, Nigeria, Simba waliibuka na ushindi wa bao 1-0, bao lilifungwa na kiungo wake kimataifa kutoka Zambia, Cloutous Chama.

Mchezo wa marudiano unatarajiwa kuchezwa siku ya Jumamosi tarehe 5 Novemba, 2020, majira ya saa 11 jioni kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam huku ukiruhusiwa kutazamwa na mashabiki 30,000 tu.

Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema kuwa siku ya mchezo huo watakwenda na kauli mbiu ya ‘Tik Tak’ lengo sio kupata ushindi tu, bali kucheza mpira mzuri ambao utawaburudisha mashabiki wa klabu hiyo.

“Tunakwenda kuwaburudisha mamilioni ya watanzania kwenye Uwanja ambao kwetu ni machinjio kwa wageni wetu, hatuendi kucheza tu, tunakwenda na burudisha na wala hatuwadharau, Plateau ingawa tumewafunga kwenye mchezo uliopita,” alisema Manara.

“Hatuendi kucheza michuano hii kama hisani, tunakwenda kucheza kama mabingwa mara baada ya kuchukua ubingwa wa msimu uliomalizika kwa hiyo lazima tuwakilishe nchi kwenye mashindano ambayo tumeyataka” aliiongezea Haji Manara

Tiki Taka ni aina mpira wa kihispania ambao sifa yake kubwa ni kumiliki mpira kwa  kupiga pasi fupi fupi huku timu ikiwa inatembea kwenda kushambulia na mara nyingi aina hii ya mpira hutumika na klabu ya FC Barcelona ya Hispania.

Simba inaingia kwenye mchezo huo wa marudiano siku ya Jumamosi huku ikiwa na kumbukumbu ya kuondoshwa kwenye michuano hii katika hatua ya awali kwenye msimu uliopita dhidi ya UD Songo kutoka Msumbiji mara baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1.

Viingilio kwenye mchezpo huo vitakuwa Tsh. 150,000 kwa Platinum, VIP A Tsh. 40,000, VIP B na C Tsh. 20,000 huku mzunguko ikiwa ni Tsh. 7,000.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!