Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tibaijuka azungumzia sekeseke la utekaji
Habari za SiasaTangulizi

Tibaijuka azungumzia sekeseke la utekaji

Anna Tibaijuka, aliyekuwa Mbunge wa Muleba Kusini
Spread the love

MBUNGE wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka amewataka watanzania kuwa makini kuhusu usalama wao kutokana na uwepo wa makundi ya wahuni na watekaji wanaojaribu kutaka kuvuruga amani iliyopo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tibaijuka ameyasema hayo wakati akizungumza na vijana 177 waliohitimu mafunzo ya mgambo (jeshi la akiba) katika Kata ya Kalambi jimboni Muleba Kusini.

“Wananchi tukae mkao wa kudadisi mambo, ukiona mtu haeleweki humjui toa taarifa, ukiona kifurushi kimewekwa mahali usiwe mwepesi kuangalia nini usikute bomu limetegeshwa. Watu wabaya sana, wanataka kuharibu amani iliyopo kuivuruga,” amesema Prof. Tibaijuka.

Kuhusu vijana hao wa jeshi la akiba, Prof. Tibaijuka amesema kuna mpango wa kufunguliwa kampuni ya ulinzi ili vijana hao wapate ajira sambamba na kuimarisha ulinzi na usalama jimboni mwake hasa bomba la mafuta la Tanzania na Uganda linalotokea Tanga hadi Hoima nchini Uganda.

Vile vile ametoa ametoa fedha kwa ajili ya kununua sare za vijana hao walio maliza mafunzo jimboni kwake.

“Nilikua nawakumbusha miadi yetu kwamba tunakwenda kufungua kampuni ya ulinzi kusudi iwasaidie kupata ajira. Mimi kama mbunge wao lazima niwasaidie lakini huwezi pata ajira kabla ya kuweka miundombinu ya ajira.

Sasa ulinzi ni lazima, lazima uwe na vyombo vya ulinzi, ndio maana nakazana waunde kampuni, ulinzi umekuwa biashara ni fani inayopanuka sababu wahuni wamekuwa wengi, watekaji na kadhalika. Bomba letu la mafuta Rais John Magufuli amelileta na sisi angalau tuliunge mkono kwa kulilinda “amesema Prof. Tibaijuka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!