Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko THDRC yamfuata mwandishi Kabendera polisi
Habari Mchanganyiko

THDRC yamfuata mwandishi Kabendera polisi

Erick Kabendera
Spread the love

MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THDRC), umetuma wawakilishi wake kupeleka maombi ya dhamana kwa mwandishi Erick Kabendera. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Jeshi la Polisi leo limeeleza, linamshikilia mwandishi huyo wa habari za uchunguzi ndani na nje ya nchi. Limeeleza kuwa lina wasiwasi na uaria wake.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 30 Julai 2019 na THDRC imeeleza, mawakili wake Jones Sendodo, Shilinde Swedy na Catherine Ringo wamepeleka maombi ya dhamana ya Kabendera mahakamani.

Taarifa ya mtandao huo inaeleza, maombi hayo ya dhamana Namba 14 ya mwaka 2019, yamepangwa mbele ya Hakimu Mwandamizi Rwizile na kusikilizwa Alhamisi ya tarehe 01 Agosti 2019.

“Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu umechukua hatua ya kupeleka maombi ya dhamana mahakamani, baada ya kufuatilia jana vituo vya polisi Oysterbay na Central na kuambiwa kwamba Erick hakuwepo katika moja ya vituo tajwa hapo juu,” inaeleza sehemu ya taarifa ya THRDC.

Kabendera alikamatwa na jeshi la polisi jana tarehe 29 Julai 2019 jioni. waliomkamata walivamia nyumbani kwake Mbweni na kuondoka naye.

“Tangu akamatwe, Erick hajapata nafasi ya kuwasiliana na wakili wake wala ndugu zake wa karibu,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!