SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limesongeza mbele mechi kati ya Tanzania Prisons dhida ya Biashara United iliyokuwa ichezwe kesho Jumanne tarehe 19 Oktoba 2021. Anaripoti Damas Ndelema, TUDARCo … (endelea).
Mchezo huo uliokuwa upigwe dimba la Nelson Mandela, Sumbawanga, mkoani Rukwa, umesogezwa mbele ili kuwapa fursa Biashara United kujiandaa kwa mchezo wao wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Al Ahaly Tripoli ya nchini Libya.
Katika mchezo wa kwanza uliopigwa mwishoni mwa wiki katika Uwanja wa Benjami Mkapa jijini Dar es Salaam, Biashara waliibuka na ushindi wa 2-0.
Taarifa ya meneja wa Biashara United ya mkoani Mara, Frank Wambare aliyoitoa leo Jumatatu tarehe 18 Oktoba 2021, imeeleza wameipokea taarifa hiyo vizuri na kwa furaha na wataitumia vizuri nafasi hiyo kujiandaa vya kutosha iliwaweze kupata ushindi wa ugenini na kufuzu hatua inayofuata.
Pia, mda huo watatumia kushughulikia mambo ya usafiri kwani wanatarajia kuondoka nchini keshokutwa Jumatano au Alhamisi kwa ndege ya kuunga kwani hakuna ndege ya moja kwa moja. Aidha amesema, kambi inaendelea jijini Dar es Saalam.
Leave a comment