Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo TFF yapangua tena ratiba ya Ligi Kuu Bara
Michezo

TFF yapangua tena ratiba ya Ligi Kuu Bara

Spread the love

MICHEZO namba 14 na 19 ya Ligi Kuu Bara kati ya mabingwa watetezi Simba na Mbeya City na ule wa Azam FC dhidi ya Ndanda itachezwa siku ya Jumatatu 27 Agosti, 2018 badala ya 25 Agosti, 2018 kama ilivyopangwa hapo awali kutokana na mabadiliko yaliyofanywa na bodi ya ligi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Katika sehemu ya barua iliyotoka bodi ya ligi iliyosainiwa na Mwenyekiti wake Boniface Wambura imeonesha sababu za kusogeza michezo hiyo mbele ni kupisha maandalizi ya mchezo wa fainali wa kombe la CECAFA U-17.

“Mabadiliko haya yametokana na Uwanja wa Taifa kufanyika maandalizi kwa mchezo wa fainali za CECAFA U-17 ambao utachezwa tarehe 26.08.2018 (Jumapili)”

Hii ni mara ya pili kwa bodi ya ligi kupangua michezo ya Ligi Kuu kwa msimu huu wa 2018/19 kutokana na sababu za kuingiliana kwa shughuli za matumizi ya viwanja na hali hiyo inatokea kutokana na 90% ya klabu zinazoshiliki ligi hiyo havina viwanja vyao binafsi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!