Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo TFF yafungua siku 42, dirisha la usajili
Michezo

TFF yafungua siku 42, dirisha la usajili

Ofisi za TFF
Spread the love

 

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefungua rasmi dirisha kubwa la usajili litakalodumu kwa siku 42, baada ya kumalizika kwa msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2020/21. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Dirisha hilo la usajili litahusu timu ziunazoshiriki Ligi Kuu. Ligi daraja la kwanza na la pili pamoja na Ligi Kuu ya wanawake.

Katika taarifa iliyotolewa na TFF, imeeleza kuwa dirisha hilo, limefunguliwa kuanzia leo tarehe 19 Julai, 2021 na litafungwa tarehe 31 Agosti, 2021.

Wakati taarifa hiyo ikitoka tayari klabu mbalimbali za Ligi tayari zilishaanza usajili wakati msimu ukielekea mwishoni.

Klabu za Simba, Yanga na Azam FC tayari walishaanza kufanya hivyo kwa kuwasainisha baadhi ya wachezaji kwa mikataba ya awali.

Mpaka sasa klabu ya Yanga imeshakamlisha usajili wa beki wa kulia kutoka Jamhuri ya Congo, Djuma Shaban ambaye alikuwa anakipiga kwenye klabu ya AS Vita.

Kwa upande wa Azam FC wao mpaka sasa wamekamilisha usajili wa wachezaji wawili kutoka Zambia, ambao ni Charles Zulu, aliyekuwa anakipiga kwenye klabu ya Cape Town City inayoshiriki Ligi Kuu nchini Afrika Kusini na mwengine ni Paul Katema kutoka kwenye klabu ya Red Arrows.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!