Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo TFF yafikishwa Mahakamani
MichezoTangulizi

TFF yafikishwa Mahakamani

Walace Karia, Rais wa TFF
Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imepokea kesi ya kupinga uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), iliyofunguliwa na Ally Saleh ‘Alberto’ ambaye alikuwa moja ya wagombea kwenye uchaguzi huo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Uchaguzi huo ulipangwa kufanyika tarehe 8 Agosti, 2021, jijini Tanga, ambapo mpaka sasa kamati ya uchaguzi imempitisha Wallace Karia kuwa mgombea pekee kwenye nafasi ya Urais.

Ally Saleh ‘Alberto’

Kesi hiyo ya madai namba 98 ya mwaka 2021, iliyofunguliwa na Ally Salehe, raia wa Tanzania anayeishi Zanzibar ambayo itakuwa chini ya Jaji Kakolaki ambapo wadai ni TFF, Bodi ya wadhamini na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Wakili Kiomoni Kibamba.

Mahakama hiyo pia imewataka wadaiwa hao wote watatu kufika kesho mahakamani hapo, kujibu hoja ya kwanini uchaguzi huo usisimamishwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

error: Content is protected !!