SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linavikumbusha klabu za Ligi Kuu, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili ambavyo havijafanya usajili kupitia mfumo wa usajili wa TFF FIFA Connect kufanya usajili wao. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Klabu ambazo bado hazijafanya usajili wawasiliane na TFF kama kuna msaada wowote wanahitaji ili kukamilisha usajili wao.
Dirisha la Usajili litafungwa Alhamisi Julai 26, 2018 na TFF inasisitiza hakutakuwa na muda wa ziada katika usajili.Timu ambayo itashindwa kukamilisha usajili haitaruhusiwa kushiriki Ligi ya msimu ujao wa 2018/2019.
Klabu za Ligi Kuu ambazo hazikamilisha usajili bado ni Ruvu Shooting, Mbeya City, Tanzania Prisons, Mtibwa Sugar, Mwadui, Kagera Sugar, Alliance, Lipuli, African Lyon, KMC na Azam FC.
Kwa upande wa ligi daraja la kwanza klabu ambazo hazijakamilisha usajili ni Ashanti United, Boma FC, Friends Rangers, Green Warriors, Kiluvya United, Majimaji FC, Mashujaa FC, Mawenzi Market, Mbeya Kwanza, Mgambo Shooting, Njombe Mji, Pamba FC, Dar City na Polisi Tanzania.
Klabu za daraja la pili ambazo hazijakamilisha ni Area C United, Changanyikeni, Cosmopolitan FC, Kumuyange FC, Gipco FC, Mirambo FC, Madini FC, Mkamba Rangers, Mvuvumwa, Polisi Dar, The Mighty Elephant, Toto African, Villa Squad, Majimaji Rangers, Mtwivila City, Kasulu Red Star na Sahare All Stars.
Leave a comment