KAMATI ya Sheria na Hadhi za Wachezaji wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeamua kuwa Feisal Salum bado ni mchezaji wa Yanga kwa mujibu wa mkataba. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa iliyotolewa leo tarehe 7 Januari, 2023 na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Mario Ndimbo imesema uamuzi kamili kwa pande zote mbili zilizokuwa zinahusika katika shauri utatolewa Jumatatu tarehe 9 Januari, 2023.
Klabu ya Yanga iliwasilisha malalamiko mbele ya kamati hiyo ikipinga hatua ya mchezaji wao Feisal Salum kuvunja mkataba kati yao bila kuwashirikisha.
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ilisikiliza malalamiko hayo jana ambayo pande zote (Yanga na Feisal Salum) ziliwakilishwa na wanasheria wao.
Leave a comment