Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Tetesi za Ebola: WHO yatuma mjumbe Tanzania
Habari Mchanganyiko

Tetesi za Ebola: WHO yatuma mjumbe Tanzania

Spread the love

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO), limetuma mjumbe wake Dk. Tigest Ketsela Mengestu nchini Tanzania, kwa ajili ya kufanya mazungumzo na serikali kuhusu tetesi za uwepo wa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola. Anaripoti Martin Kamote…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 24 Septemba 2019 na Dk. Hassan Abassi, Msemaji Mkuu wa Serikali, Tanzania ilimwita Dk. Mengestu ambaye anaiwakilisha WHO hapa nchini, ili kutoa maelezo kuhusu taarifa ya shirika hilo inayosambaa katika vyombo vya habari.

Hivi karibuni, ilisambaa taarifa ya WHO inayoeleza kwamba serikali ya Tanzania haitoi ushirikiano kwa shirika hilo, katika kufanya uchunguzi wa sampuli za watu wanaodaiwa kwamba wamefariki kwa ugonjwa wa Ebola.

Dk. Abbasi amekanusha madai hayo akisema kwamba, Dk. Mengestu amesema WHO haijasema na wala haina ushahidi wowote kuwa nchini Tanzania kuna Ebola.

“Serikali imemwita Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) hapa nchini kupata kwa kina hoja za Shirika hilo zinazosambaa kupitia vyombo vya habari. Mwakilishi huyo amesisitiza kuwa WHO haijasema wala haina ushahidi wowote kuwa TZ kuna Ebola na itashirikiana na Serikali,” amesema Dk. Abassi.

Dk. Abbasi ameeleza kuwa, katika mazungumzo ya Dk. Mengestu na Dk. Damas Ndumbaro, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wamekubaliana kwamba WHO itafuata taratibu husika itakapotaka taarifa zaidi kuhusu suala hilo, kutoka serikalini.

“Aidha, katika mazungumzo hayo WHO imeafiki kuwa kama kuna mahitaji ya kupata taarifa zaidi kutoka Serikali ya Tanzania lazima utaratibu ulioanishwa katika miongozo ya taasisi hiyo na ambayo imeridhiwa na Serikali ifuatwe kikamilifu,” amesema Dk. Abassi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB yakabidhi vifaa vya ujenzi, samani kwa shule ya msingi Sinyaulime, Chuo cha FDC Morogoro

Spread the loveBENKI ya NMB imekabidhi vifaa vya ujenzi kwa shule ya...

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

error: Content is protected !!