Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Tetemeko la ardhi Uturuki: Vifo vyaongezeka hadi 4,800
Kimataifa

Tetemeko la ardhi Uturuki: Vifo vyaongezeka hadi 4,800

Spread the love

 

Idadi ya vifo vilivyotokana na tetemeko lililotokea jana Jumatatu katika mpaka wa Syria na Uturuki, imeongezeka hadi kufikia zaidi ya 4,800 bada ya waokozi kuendelea na zoezi hilo usiku kucha. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Waokozi hao wanawatafuta watu walio chini ya kifusi baada ya tetemeko hilo la ardhi ambapo hadi sasa Uturuki imethibitisha vifo 2,379 huku Syria ikirekodi vifo zaidi ya 1,400.

Shirika la Afya Duniani (WHO) linakadiria kuwa yamkini waliokufa ni mara nane zaidi ya idadi inayojulikana hivi sasa.

Wizara ya Afya ya Uturuki imesema kuwa magari ya kubeba wagonjwa yapatayo 813 yamepelekwa katika maeneo yaliyoathirika, na vikundi maalumu vya huduma za dharura zaidi ya 220 vimeambatana na magari hayo.

Tetemeko hilo lenye ukubwa wa 7.8 kwenye kipimo cha Richter liliitikisa sehemu ya katikati mwa Uturuki na kaskazini mwa Syria alfajiri ya jana, na kufuatiwa na jingine dakika 10 baadaye, likiharibu vibaya miundombinu katika miji ipatayo 12.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!