WATU 300 wamefariki dunia katika tetemeko kubwa la ardhi lenye kipimo cha 7.8, lililotokea leo tarehe 6 Februari 2023, katika mpaka wa nchi ya Uturuki na Syria. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Kwa tukio hilo, imeelezwa kuwa zaidi ya watu 50 katika idadi hiyo wamefariki dunia upande wa Syria.
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki, Suleymon Soylu, amesema miji 10 nchini humo imeathirika na tetemeko hilo, ikiwemo Gaziantep, Kahramanmaras, Hatay, Osmaniye, Adiyaman, Malatya, Sanliurfa.
Pia imeripotiwa kuwa majengo mengi yameporomoka na kwamba timu za uokoaji zimetumwa kutoa msaada kwa manusura wa tetemeko hilo.
Leave a comment