Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Tetemeko jingine la ardhi laua watatu
Kimataifa

Tetemeko jingine la ardhi laua watatu

Spread the love

TETEMEKO la ardhi lenye kipimo cha 6.4 limeua watu watatu jana tarehe 20 Februari 2023 na kujeruhi wengine zaidi ya 200 katika baadhi ya maeneo ya Uturuki yaliyoharibiwa wiki mbili zilizopita na tetemeko kubwa lililoua maelfu ya watu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Majengo zaidi yaliporomoka na kuwanasa baadhi ya watu, huku kukiripotiwa idadi ya watu wengi waliojeruhiwa katika nchi jirani ya Syria.

Kitovu cha tetemeko la Jumatatu kilikuwa katika mji wa Defne, katika mkoa wa Uturuki wa Hatay, eneo lililoathirika vibaya katika tetemeko la tarehe 6 Februari 2023 la kipimo cha 7.8.

Tetemeko la Jumatatu lilisikika pia nchini Syria, Jordan, Cyprus hata nchini Misri, likifuatiwa na tetemeko la pili la kipimo cha 5.8.

Waziri wa mambo ya ndani wa Uturuki Suleyman Soylu amesema watu watatu waliuawa na 213 kujeruhiwa.

Juhudi za kuwatafuta na kuwaokoa manusura zilikuwa zikiendelea katika majengo matatu yaliyoporomoka ambako watu sita wanasadikiwa wamenaswa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!