JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF), limesema linatarajia Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, atatimiza ahadi yake ya kupeleka bungeni jijini Dodoma, Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Huduma za Habari ya 2016. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Balile ametoa kauli hiyo leo Alhamisi, tarehe 19 Januari 2023, akizungumza katika ofisi za TEF zilizoko Kisutu, jijini Dar es Salaam.
“Mwezi huu tunatarajia kwamba Wizara ya Habari itawasilisha muswada wa huduma za habari bungeni kama waziri (Nape Nnauye) alivyoahidi mara kadhaa kwamba utaingia bungeni, utajadiliwa na Mungu akipenda Februari 2023 utapitishwa na kuwa sheria tuanze utaratibu mwingine wa kuunda vyombo vinavyotakiwa ikiwemo Baraza Huru la Habari na kuangalia utunzi wa kanuni zitakazotokana na mabadiliko mbalimbali,” amesema Balile.
Balile amesema kuwa, maelekezo yaliyotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan, kuhusu maboresho ya sheria za habari, yanaanza kufanyiwa kazi na hivyo muelekeo wake ni mzuri.
“Sasa tuna hamu kubwa kuona kwamba muswada huo unaingia baada ya kushindikana katika Bunge la Februari , Septemba na Novemba 2022. Lakini tulikwisha zungumza na waziri na watendaji serikalini hivyo ni matumaini yetu makubwa sana tunataraji tutauona muswada huo ukiingia bungeni na mambo yote yaweze kwenda vyema,” amesema Balile.
Serikali ya Tanzania ilichelewa kuwasilishwa Muswada huo bungeni, ili kuwapa nafasi ya kutosha wadau kutoa maoni yatakayosaidia upatikanaji wa sheria bora na rafiki kwa sekta ya habari.
Leave a comment