Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa TEF: Spika Ndugai kakosea
Habari za Siasa

TEF: Spika Ndugai kakosea

Job Ndugai, aliyekuwa Spika wa Bunge Tanzania
Spread the love

JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF), limeeleza kutofurahishwa na hatua ya Job Ndugai, Spika wa Bunge kuzuia waandishi wa habari kuzungumza na wabunge baada ya kuamua kutoka nje ya ukumbi wa bunge. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Leo tarehe 4 Aprili mwaka 2019, wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na baadhi kutoka Chama cha Wananchi (CUF) waliotoka nje wakionesha kukasirishwa na hatua ya Bunge kumwadhibu Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini kutohudhuria Mikutano mitatu ya Bunge.

Baada ya wabunge hao kutoka nje, Spika Ndugai aliagiza kuwa, wasizungumze na waandishi wa habari na kuonya kwamba, atakayefanya hivyo atachukuliwa hatua.

Adhabu hiyo ilitolewa leo baada ya Lema kuitwa kwenye kikao na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge jana kueleza sababu za kuunga mkono kauli ya Halima Mdee, Mbunge wa Kawa kwamba, Bunge ni dhaifu.

Mdee alitoa kauli hiyo akiunga mkono kauli ya Prof. Mussa Assad, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) aliyoitoa mwaka jana akiwa Marekani kwamba, Bunge ni dhaifu.

Deudatus Balile, Kaimu Mwenyekiti wa TEF amesema kuwa, Spika Ndugai amepotoka kwa kauli hiyo kutokana na kusigina ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri inayoeleza uhuru wa kujieleza na kutoa habari.

Balile amesema, “spika kazungumza hayo labda kwa sababu ya joto lakini amekosea.”

Amesema kuwa, kifungu cha saba na kifungu kidogo cha kwanza kinatambua haki ya mwanahabari hivyo, Spika Ndugai amekiuka sheria aliyoshiriki kuipitisha mwenyewe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!