Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari TCRA yawataka wasafirishaji wa vipeto kujisajili na wengine kuhuisha leseni
HabariHabari Mchanganyiko

TCRA yawataka wasafirishaji wa vipeto kujisajili na wengine kuhuisha leseni

Spread the love

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Mashariki imetoa wito kwa wadau wa posta wenye leseni kuhakikisha kuwa wanafuata taratibu, kanuni na sheria pamoja na kuhuisha leseni zao ili wafanye kazi zao kwa ufanisi na kutambulika zaidi. Anaripoti Mwandishi Wetu…..(endelea)

Hayo yameelezwa leo Jijini Dar es Salaam na Kaimu Meneja TCRA Kanda ya Mashariki Ikuja Jumanne katika utoaji mafunzo kwa wadau wa posta kupitia kampeni walioanzisha ya kutambua umuhimu wa kukata leseni na ambao bado wakate kwani itawasaidia kufanya kazi zao kwa uhuru zaidi.

Aidha amesema kuwa elimu hiyo imekuja kutokana na uwepo wa malakamiko ya wateja kupotelewa na vipeto na vifurushi vyao kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha hivyo kutapeli watu na kushindwa kujua wamdai nani.

Hata hivyo amesema kupitia kampeni walioanzisha ya “Tumachapuchapu kwa Usalama “ itawezesha elimu kuwafikia wananchi wengi kupitia vipeperushi, vyombo vya habari, vituo vya usafiri na elimu zinazoendelea kutolewa na TCRA ili kupunguza wimbi la upotevu wa vipeto na vifurushi.

Ameongeza kuwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) haihusiki tu na usimamizi wa Mawasiliano bali pia wana kitengo cha posta ambacho hushughulikia utumwaji wa vipeto vyenye kilogramu 2 na vifurushi vyenye kilogramu 30 ndani na nje ya nchi kupitia kampuni zilizosajiliwa na mamlaka hiyo.

Amesema kuwa kuanzishwa kwa kitengo hich cha posta kumewezesha ongezeko la pato la taifa kkutokana na kusajiliwa kwa nakampuni hayo ya utumaji vifurushi na vipeto pamoja na kuongeza ajira kwa watanzania.

Kwa upande wao wada wa posta walioshiriki katika mafunzo hayo wamemshukuru Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA kwa kuwapatia elimu hiyo ambayo itasaidia kutatua changamoto mbalimbali walizokuwa wanakumbana nazo wakati wa utumaji wa vipeto na vifurushi.

Hatahivyo wameiomba Mamlaka hiyo kuendelea kushirikiana na wadau hao wa posta katika kukabiliana na wimbi la watu wasiofuata taratibu za usajili ambao huwasababishia usumbufu pindi mteja anapopoteza kipeto au kifurushi na kushindwa kujua amdai nani kwani aliowapa watume hawajasajiliwa.

Meneja wa Basi la Gallaxy Magreth Kibiki amesema kuwa wapo watu hawana mabasi lakini wanafanyabiashara ya kusafirisha vipeto na kuleta usumbufu kwao wakati mzigo umepotea na kudai walipwe wakati hawana stakabadhi ya malipo ya basi husika.

Kibiki amesema wananchi wanatakiwa kuwa na uangalifu wa kutuma mizigo kwenda katika kampuni ambazo zinafanya biashara kwa ya kusafirisha vipeto kwa njia ya halali.

Afisa Mauzo na Masoko wa ATCL Hellon anasema kuwa wanapata changamoto na matepeli wanawatumia ujumbe mfupi kuwatumia watu kuwa na mzigo ATCL wakiomba watume fedha ambapo waliotumiwa ujumbe wanatuma na kuanza kufatilia ATCL kupatiwa mzigo na kuleta usumbufu kwao.

Amesema kuna baadhi wanasafirisha mizigo kwenda nje wanatumia mwanya wa abiria wasio na mizigo hali amabayo ni changamoto kwa wenye leseni kukosa kufanya biashara na hao baadhi ya watu wanaotumia fursa isiyo halali kwao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!