Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA yabariki ongezeko bei za bando, wasema ni jambo la kawaida
Habari MchanganyikoTangulizi

TCRA yabariki ongezeko bei za bando, wasema ni jambo la kawaida

Spread the love

 

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema mabadiliko ya bei za bando iliyofanywa na baadhi ya kampuni za simu za mkononi nchini ni jambo la kawaida katika soko la ushindani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya bei ya bando hizo kupanda ghafla na kuibua malalamiko kwa mara nyingine kwa watumiaji wa huduma hizo nchini.

Mathalani aliyekuwa akinunua bando la Tigo la mwezi kwa Sh. 20,000 alikuwa akipatiwa dakika, sms na GB10 lakini sasa anapata GB 6.5. Aliyekuwa akijiunga bando la Sh. 35,000 kwa mwezi alikuwa akipata GB30 lakini sasa ni GB 25.

Mabadiliko kama hayo yamefanywa pia na kampuni ya Airtel ambapo mtumiaji alikuwa akipata GB 1 na dakika kadhaa kwa siku tatu kwa gharama ya Sh 1,000 lakini sasa ni mteja anapatiwa MB 500 pekee.

Aidha, kutokana na mabadiliko hayo ambayo yametokea pia katika mitandao mingine ya kampuni za simu za mkononi nchini, MwanaHALISI Online imezungumza na Mkurugenzi wa Masuala ya Sekta wa Mamlaka hiyo, Dk. Emmanuel Manasseh kuhusu mabadiliko hayo.

Akizungumzia mabadiliko hayo leo Jumatatu tarehe 4 Oktoba 2021, Mkurugenzi huyo amesema sheria na kanuni hazimzuii mtoa huduma kubadilisha bei za vifurushi hivyo.

Mkurugenzi wa Masuala ya Sekta wa Mamlaka TCRA, Dk. Emmanuel Manasseh

“TCRA kazi yetu ni kusimamia gharama, bei za huduma za mawasiliano lakini sheria na kanuni zetu hazimfungi mtoa huduma kubadilisha bei zake. Soko letu ni la ushindani si la mtu mmoja.”

“Mabadiliko ya bei hayakuanza leo au jana, bei za bando za mwaka 2011 si kama za sasa ambazo zimepungua,” amesema.

Alipoulizwa, kama kuna dokezo limeletwa kabla ya kuipitisha, Dk. Manaseh amesema kampuni hizo za simu zilipeleka na baada ya TCRA kuzipitia waliona ziko sahihi na hawakuona sababu ya kuzizuia.

Dk. Manasseh amesema, mabadiliko ya awali ambayo bei za bando zilipanda kisha zikarejeshwa kama awali, utaratibu wake haukufuatwa.

“Kwa sababu mtoa huduma haruhusiwi kubadili vifurushi vyote, ndivyo ilivyokuwa tofauti na sasa,” amesema.

Ameongeza kuwa katika biashara kubadilisha bei kwenye soko la ushindani ni jambo la kawaida.

“Mtoa huduma anaweza kubadilisha bei akaona haiendani na soko anarudi kwetu kutuambia hii naibadili na sisi tunaona yuko ndani ya utaratibu tunamruhusu,” amesema.

6 Comments

  • Mamlaka ya TCRA haifanyyi kazi ipasavyo. It is part of communication companies that overnight generating profits out of the citizens. The President should take action against this important government authority. Siamini kama wasimamizi wa mamlaka hii ni sehemu ya maslahi ya wananchi.

  • Sasa kama nyie hamumzuii mtoa huduma kupandisha bei anapojisikia,hamuoni kama kuwepo kwenu ni kula kodi zetu bila sababu?na hamuoni kama hamstahili kuwep?

  • This institution has failed according to them that they had no option for them to block these companies raise the tariff at anytime they want.We as tanzanians think it’s now right time for our President to demolish these govt institution s which does not help the citizens but they are for the interest of investers

  • Ukisoma Sheria ya TCRA inaonesha kuwa wanajukumu pia la kuhakikisha ushindani kwenye soko. Tumeona mara Nyingi watoa huduma wakipewa adhabu kwa kutoa huduma zisizo na viwango vinavyokidhi. Nadhani TCRA wanajaribu kusimamia Misingi ya Sheria kwa kuwalinda Watumiaji wa huduma pamoja na katoa huduma. Mimi kam mteja ningependa huduma za Mawasiliano zile bure; Mtoa huduma angependa kupata faida kutoka kwenye huduma; na Serikali inaangalia watanzania wapate huduma bora kwa bei nafuu na pia Serikali ipate kodi. Tumewaelewa kuhusu suala la bei lakini tunaomba msimamie ubora wa huduma. Bado ubora wa huduma hauridhishi.

  • Kwa kweli si kila kifurushi kimepanda bei, cha kwangu wamepunguza data kidogot wakaongeza dakika za maongezi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!