Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko TCE yazindua kampeni ya malezi chanya
Habari Mchanganyiko

TCE yazindua kampeni ya malezi chanya

Spread the love

TAASISI inayoshughulika na masuala ya maendeleo na ustawi wa jamii (TCE), imezindua kampeni ya malezi chanya, kwa ajili ya kukabiliana na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika leo tarehe 18 Julai 2019 jijini Dar es Salaam, Rahim Ndambo, Mkurugenzi Mtendaji wa TCE amesema lengo la kampeni hiyo ni kuhamasisha wazazi, walezi na jamii kwa ujumla, kutimiza wajibu wao katika kulinda haki za watoto.

Ndambo ameeleza kuwa, TCE imeamua kuanzisha kampeni hiyo, baada ya kubaini ongezeko la vitendo vya ukatili kwa watoto, huku miongoni mwa sababu zinazochochea changamoto hiyo, ni wazazi na walezi, kutotimiza jukumu lao la kulea watoto.

“Lengo la kampeni hii ni kuanzisha jitihada na mkakati endelevu,  zenye matokeo, ili kuwafahamisha wazazi,walezi, serikali na jamii kwa ujumla kuwa unyanyasaji huu unatokana na kutokua na malezi chanya katika familia zetu,” amesema Ndambo.

Ndambo ameeleza kuwa, wazazi na walezi wengi nchini wanasahau misingi sahihi ya malezi ya watoto kutokana na kubanwa na majukumu ya kazi, na kuwaacha wafanyakazi za ndani ambao hawana ujuzi wa malezi ya watoto.

“Hatari kubwa imekuwa ikionekana mbeleni, maana vitendo hivi  hutokea katika maeneo ya kuaminika na  salama kabisa  kwa watoto  kama nyumbani, shuleni, nyumba za ibada, vyombo vya usafiri  na hata kwenye mtandao ya kijamii, kama kutishwa au kushawishiwa ikiwa ni njia ya mtego wa kuweza kuwanasa watoto,” amesema Ndambo.

Marry Mangu, Mratibu wa TCE amesema kampeni hiyo itafanyika katika mikoa 8 iliyoathirika zaidi na vitendo vya unyanyasaji wa watoto.

Mangu ametaja mikoa hiyo ikiwemo, mkoa wa Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Simiyu, Arusha, Kilimanjaro, Tabora na Singida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

error: Content is protected !!