Tuesday , 30 May 2023
Home Habari Mchanganyiko TCAA watakiwa kufuata kanuni za kazi
Habari Mchanganyiko

TCAA watakiwa kufuata kanuni za kazi

Spread the love

SERIKALI aimeitaka Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na sheria za nchi katika utendaji wake wa kazi. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Hayo yalisemwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasailiano Prof. Makame Mbarawa, wakati alipokuwa akizindua Baraza la wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) mjini Dodoma.

Amesema ili kufikia malengo na mafaniko ya shirika hilo ni lazima wafanyakazi wote wanatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni, taratibu na sheria za nchi katika kutimiza majukumu yao ya kila siku.

Aidha amesema kuwa TCAA haiwezi kufanikiwa kama hapatakuwepo na uwajibikaji wa wafanyakazi wake katika kusimamia sheria na kanuni za nchi zilizowekwa.

“Kwa mwaka uliopita tu anga yetu ilitumiwa na wasafiri zaidi ya milioni 4.1 ambao walitumia anga yetu kwa maana hiyo basi kama tunataka kuongeza watu ambao wanatumia naga yetu kusafiri basi tuhakikisha tuanaendelea kusimamia kazi zetu kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi,” amesema Makame.

Vilevile aliwataka wafanyakazi wa shirika hilo kuacha kulalamikia maslahi yao binafsi wakati wanashindwa kutimiza majukumu yao waliyopewa katika nafasi zao.

“Leo hii hamuwezi kulalamikia kutaka kupandishiwa mishara wakati nyinyi wenyewe mmeshindwa kuzalisha wala hamkusanyi mapato ya kutosha,” amesema.

Amesema kama watumishi hao wa TCAA wataweza kufanya kazi kwa kujituma na kusiamamia mapato katika maeneo yao hakuana anatakeye pinga wao kupandishiwa mishahara.

“Leo hii mshindwe kukukusanya mapatao ya kutosha halafu nisikie kuwa mmepandishiwa mishara yenu nitamuondoa mara moja kwenye nafasi yake Mkurugenzi wenu mkuu Bwana Hamza maana atakua ahafai, fanyeni kazi hakuna anataye wanyima maslahi yenu,” amesisitiza Prof. Makame

Pia amelipongeza shirika hilo kwa kufanikiwa kununua Rada mpya kwa fedha zake bila kukopa benki hali ambayo katika kipindi cha nyuma ilikuwa ni vigumu.

“Rada ya mwisho kununuliwa ilikuwa ni mwaka 2002 lakini niwapongeze kwa kununua nyingine kwani mlikuwa mkitegemea serikali ndio itoe fedha kwajili ya hii rada lakini kumbe hata nyine mnaweza kwa kutumia mapato yenu wenyewe,” amesema.

Naye Mkurugenzi mkuu wa TCAA Hamza Johari amesema kuwa lengo la kuwa na baraza hilo la wafanyakazi ni kuhakikisha kuwa wanaibua mikakati mikubwa ya kimaendeleo katika sekta ya usafiri wa Anga.

Hata hivyo amesema pia katika chuo kinacho toa mafunzo ya usafiri wa anga wameendelea kupokea wanafunzi wengi kutoka nje ambao wanasaidia kuongeza mapato.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wenye ulemavu waiomba MISA-TAN iwajengee uwezo wa uhuru wa kujieleza

Spread the love  TAASISI ya vyombo vya Habari kusini mwa Afrika (MISA-TAN)...

Habari Mchanganyiko

Wanawake wajawazito 2000 Korogwe washiriki Marathon, Mwenyekiti UWT amsifu Jokate

Spread the loveWANAWAKE wajawazito zaidi ya 2000 wilayani Korogwe mkoani Tanga wameshiriki...

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

error: Content is protected !!