Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TBS yapiga ‘stop’ tairi zilizotumika
Habari Mchanganyiko

TBS yapiga ‘stop’ tairi zilizotumika

Spread the love

SHIRIKA la Viwango Nchini (TBS) limepiga marufuku matumizi ya tairi za vyombo vya moto zilizotumika na kuisha muda wake. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 24 Oktoba 2018 na TBS kupitia Mkurugenzi Mkuu wake, Dk. Ngenya Yusuf.

“TBS inapenda kuwakumbusha waagizaji na watumiaji wa tairi za magari kuwa umri wa tairi za magari ni miaka nane kutoka tarehe ya kutengenezwa kwake ambayo imeanishwa katika kila tairi. Tairi halitafaa kutumika baada ya umri huo bila kujali kuwa halijawahi kutumika kabisa,” inaeleza sehemu ya taarifa ya TBS.

Sambamba na marufu hiyo, TBS imepiga marufuku wauzaji, wasambazaji na watumiaji wa tairi za magari, pikipiki na baiskeli, kuuza na kutumia tairi hizo zilizotumika.

Vile vile, TBS imetangaza kufanya msako katika maduka ya tairi ili kubaini wauzaji watakao kiuka agizo hilo kwa ajili ya kuwachukulia hatua za kisheria.

Tangazo hili litaenda sambamba na ukaguzi utakaofanyika kwenye soko kwa lengo la kubaini watakao kiuka agizo hili kwa kuendelea kufanya biashara ya kuuza au kusambaza tairi ambazo zilishatumia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!