BARAZA la Mitihani la Tanzania (NECTA) leo Alhamisi limetangaza matokeo ya darasa la saba ambapo jumla ya watahiniwa 1,730,402 kati ya watahiniwa 1,348,073 wenye matokeo ambao ni sawa na asilimia 79.62 wamefaulu ambako wamepata madaraja A, B, C. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kaimu Katibu Mtendaji wa NECTA, Athumani Salumu amesema kati ya waliofaulu, wasichana ni 558,825 sawa na asilimia 78.91 ya wasichana wenye matokeo na wavulana ni 514,577 sawa na asilimia 80.41 ya wavulana wenye matokeo.
Akitangaza matoke ohayo jijini Dar es Salaam, Salumu amesema; “Ikilinganishwa na mwaka 2021, kitakwimu kuna punguo la ufaulu kwa asilimia 2.35 japokuwa idadi ya watahiniwa waliofaulu imeongezeka kwa 165,600 sawa na asilimia 18.24 ikilinganishwa na mwaka 2021,” NECTA.
Aidha, NECTA imefuta matokeo yote ya watahiniwa 2,194 sawa na asilimia 0.16 ya watahiniwa milioni 1.35 waliofanya mitihani, ambao wamebainika kufanya udanganyifu katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2022.
Leave a comment