Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Habari Taratibu Watanzania nje ya nchi kupiga kura hazijakamilika
HabariHabari Mchanganyiko

Taratibu Watanzania nje ya nchi kupiga kura hazijakamilika

Sanduku la kura
Spread the love

SERIKALI imesema, bado inaangalia uwezekano kwa Watanzania waishio nje ya nchi, kupiga kura katika chaguzi mbalimbali zijazo. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 23 Mei 2019, bungeni jijini Dodoma na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakati akijibu swali la Asha Abdul Juma, mbunge viti maalum (CCM)  aliyehoji, lini serikali itakamilisha utaratibu wa kuwezesha Watanzania wanaoishi nje kupata nafasi ya kupiga kura?

Akijibu swali hilo Waziri Majaliwa amesema, serikali inaendelea kuona kama utaratibu uliopo sasa unafaa kwa Watanzania hao kupiga kura.

Hata hivyo, amesema kabla ya kuruhusu raia hao kupiga kura, serikali itafuatilia mienendo ya Watanzania waishio nje ya nchi ikiwemo shughuli zao na kama bado wana uraia wa Tanzania au wameomba uraia wa nchi husika walizoko.

“Jambo hili ni la kisera, serikali imeendelea kuona utaratibu huo kama unaweza kufaa.  Sababu lazima tupate kujua nani yuko nje ya nchi, wanafanya shughuli gani na kama ni bado Watanzania au waliomba uraia wa nchi za nje.

“Na pindi sera hii itakapokamilika tutakapoona inafaa, tutakuja kujulisha Bunge na Watanzania pale inapofaa,” amesema Waziri Majaliwa.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!