Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania, Zambia kujenga bomba mafuta safi Dar-Ndola
Habari Mchanganyiko

Tanzania, Zambia kujenga bomba mafuta safi Dar-Ndola

January Makamba, Waziri wa Nishati
Spread the love

SERIKALI imetenga Sh. 500 milioni katika mwaka wa fedha 2022/23 kwaajili ya kuanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta safi kutoka Dar es Salaam hadi Zambia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yamebainshwa na Waziri wa Nishati, Januari Makamba leo Jumatano tarehe 1 Juni, 2022 akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2022/23.

Makamba amesema kazi zitakazofanyika ni kufanya mapitio ya nyaraka za mradi; kuanza taratibu za kumpata Mshauri Mwelekezi wa kufanya Upembuzi Yakinifu wa mradi pamoja na Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii zitokanazo na utekelezaji wa mradi.

Waziuri huyo amesema bomba hilo lenye urefu wa takribani kilomita 1,710 litatumia mkuza wa Bomba la kusafirisha mafuta ghafi la TAZAMA.

Aidha amesema Bomba litamilikiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Zambia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!