Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania yatangaza kushiba chakula
Habari Mchanganyiko

Tanzania yatangaza kushiba chakula

Mahindi
Spread the love

SERIKALI  imesema kuwa Taifa kwa sasa linajitosheleza kwa chakula kwa asilimia 120 kulingana na tathmini iliyofanyika mwaka huu, anaandika Mwandishi wetu.

Kauli hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki na Waziri  wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Charles Tizeba  katika mashindano ya mifugo kitaifa yanayofanyika uwanja maonesho ya Nanenane Nzuguni, mjini Dodoma.

Anasema kutokana na tathmini iliyofanyika katika msimu huu wa kilimo inaonesha kuwa Tanzania inajitosheleza kwa chakula kwa asilimia 120.

“Kwa sasa chakula kilichopo kinatutosha sasa wale watanzania wenye tabia ya kuuza chote na kwenda kwa Wakuu wa mikoa au wilaya kusema hawana chakula taratibu huo haupo,”anasema Tizeba

Anawataka kutouza chakula chote kwani kufanya hivyo ni kusababisha familia kuwa na uhaba wa chakula.

“Utaona mtu ana gunia nne halafu anazipeleka zote sokoni kwa kutegemea kuliamsha mbele ya safari, halitaamka,” alisisitizaTizeba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!