Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tanzania yapekuwa mikataba ya misaada
Habari za Siasa

Tanzania yapekuwa mikataba ya misaada

Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Profesa Adelardus Kilangi
Spread the love

 SERIKALI ya Tanzania kupitia Ofisi ya Mwansheria Mkuu (AG), inapitia upya mikataba ya misaada na mikopo takribani 70, ili kuangalia masharti yake kama yana tija kwa taifa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk. Adeladius Kilangi wakati akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Sheria yaliyofanyika leo tarehe 6 Februari jijini Dar es Salaam.

AG Kilangi ameeleza kuwa, ofisi yake inarejea mikataba hiyo ili kuangalia kama masharti yake  yana tija kwa taifa, ikiwemo sharti la kusamehe mambo mbalimbali.

“Ofisi ya AG inafanya rejea pia,  kwenye baadhi ya mikataba ya misaada na mikopo ipatayo 70.  Ili kuangalia tija ya baadhi ya masharti ikiwiemo sharti la ksuamehe mambo mbalimbali,” amesema AG Kilangi.

Wakati huo huo, AG Kilangi amesema ofisi yake imepitia upya mikataba 13 ya uwekezaji, utafutaji na uzalishaji mafuta na gesi., na kwamba imekwishawasilishwa kwa Mwanasheria Mkuu.

Pia, Ofisi ya AG imepitia mikataba 182 ya uwekezaji yenye utata, kati ya wawekezaji na mashirika ya umma.

“Hivi karibuni ofisi ya mwanasheria mkuu itaanza kurejea mikataba yote ya uwekezaji, kati ya nchi mbili na uwekezaji katika ya nchi mbalimbali ambayo inaihusu Tanzania, “ amesema AG Kilangi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!