Saturday , 10 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Tanzania yaita wawekezaji zao la Korosho
Habari MchanganyikoTangulizi

Tanzania yaita wawekezaji zao la Korosho

Spread the love

KITUO cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimetoa wito kwa wawekezaji wa ndani na wa nje ya nchi wenye nia ya kuwekeza katika zao la korosho, kushiriki katika jukwaa linalotarajiwa kufanyika kuanzia Julai 12-13, 2019 mkoani Mtwara. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Jana tarehe 21 Juni 2019 TIC  kilitoa mwaliko kwa wawekezaji watakaohitaji kushiriki katika jukwaa la korosho, ambapo Rais John Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Kwa mujibu wa mwaliko huo, jukwaa la Korosho linalenga kuwavutia wawekezaji kutoka nje ya Tanzania na wawekezaji wa ndani, katika uanzishwaji wa viwanda vya uongezaji thamani zao la korosho hasa katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

Vile vile, katika jukwaa hilo washiriki watapata fursa ya kusikia mada kutoka kwa maafisa wakuu wa serikali ikiwemo Rais Magufuli,  pamoja na kufanya mazungumzo na majadiliano na wataalamu wa zao hilo pamoja.

Fursa zilizotangazwa katika uwekezaji wa korosho, ni pamoja viwanda vya uongezaji thamani korosho ghafi, uanzishwaji wa mashamba makubwa ya korosho, biashara ya usambazaji wa vifaa na vipuri vya mitambao ya mashine za kuongeza thamani korosho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

BiasharaTangulizi

TLS wajitosa sakata la ukodishaji wa bandari

Spread the love  CHAMA cha wanasheria Tanzania (TLS), kimejitosa katika sakata la...

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

error: Content is protected !!