Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania yaita wawekezaji zao la Korosho
Habari MchanganyikoTangulizi

Tanzania yaita wawekezaji zao la Korosho

Spread the love

KITUO cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimetoa wito kwa wawekezaji wa ndani na wa nje ya nchi wenye nia ya kuwekeza katika zao la korosho, kushiriki katika jukwaa linalotarajiwa kufanyika kuanzia Julai 12-13, 2019 mkoani Mtwara. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Jana tarehe 21 Juni 2019 TIC  kilitoa mwaliko kwa wawekezaji watakaohitaji kushiriki katika jukwaa la korosho, ambapo Rais John Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Kwa mujibu wa mwaliko huo, jukwaa la Korosho linalenga kuwavutia wawekezaji kutoka nje ya Tanzania na wawekezaji wa ndani, katika uanzishwaji wa viwanda vya uongezaji thamani zao la korosho hasa katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

Vile vile, katika jukwaa hilo washiriki watapata fursa ya kusikia mada kutoka kwa maafisa wakuu wa serikali ikiwemo Rais Magufuli,  pamoja na kufanya mazungumzo na majadiliano na wataalamu wa zao hilo pamoja.

Fursa zilizotangazwa katika uwekezaji wa korosho, ni pamoja viwanda vya uongezaji thamani korosho ghafi, uanzishwaji wa mashamba makubwa ya korosho, biashara ya usambazaji wa vifaa na vipuri vya mitambao ya mashine za kuongeza thamani korosho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!