Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tanzania, Saudi Arabia kukuza ushirikiano wa kibiashara, utalii
Habari za Siasa

Tanzania, Saudi Arabia kukuza ushirikiano wa kibiashara, utalii

Spread the love

 

NCHI ya Tanzania na Saudi Arabia, zimeahidi kukuza ushirikiano katika biashara ya mazao ya kilimo pamoja na utalii. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Ahadi hiyo ilitolewa jana tarehe 25 Mei 2021, katika mazungumzo ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia, Mwana wa Kifalme Faisal Farhan Al Saud, yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Gerson Msigwa, Rais Samia alimuahidi , Mwana wa Kifalme Faisal kwamba, Serikali yake ipo tayari kukuza uhusiano na ushirikiano wake na Saudi Arabia.

“Rais Samia amemtaka kufikisha salamu zake kwa Mfalme wa Saudi Arabia, Mtukufu Salman bin Abdulaziz Al Saud na kumhakikishia kuwa, Tanzania ipo tayari kuendeleza na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wake na Saudi Arabia, katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na ustawi wa jamii,” ilisema taarifa ya Msigwa.

Taarifa ya Msigwa ilitaja baadhi ya maeneo ambayo Rais Samia ameomba kushirikiana na Saudi Arabia, ni uimarishaji biashara ya mazao ya mifugo na uvuvi, mazao ya kilimo, kutumia fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo Tanzania na kuanzisha ofisi ya Ubalozi Mdogo wa Saudi Arabia Visiwani Zanzibar.

Kwa upande wake, Mwana wa Kifalme Faisal alimhakikishia kwamba Saudi Arabia ipo tayari kuimarisha uhusiano huo, katika maeneo mbalimbali yakiwemo biashara na uwekezaji.

“Mwana wa Kifalme Faisal, amebainisha kwamba ni muhimu kwa wafanyabiashara wa Tanzania na Saudi Arabia, kushirikiana ili kukuza biashara kati ya nchi hizi mbili, ikiwa ni pamoja kuwa safari za ndege za moja kwa moja kati ya Tanzania na Saudi Arabia, ili kukuza utalii na biashara,” ilisema taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!