Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Tanzania kuwa kituo cha matibabu ya kibingwa Afrika Mashariki
Afya

Tanzania kuwa kituo cha matibabu ya kibingwa Afrika Mashariki

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake inataka kuifanya Tanzania kuwa kituo cha matibabu ya afya ya kibingwa kwa nchi inazopakana nazo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).

Akizungumza katika hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Maweni, Kigoma, leo Jumanne, tarehe 18 Oktoba 2022, Rais Samia amesema ili kufanikisha lengo hilo, Serikali yake imetenga kiasi cha Sh. 5 bilioni kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Kanda mkoani humo.

“Kama nilivyosema Kigoma ni mkoa wenye watu wengi lakini uko pembezoni mwa Tanzania umepakana na nchi jirani na sisi maono yetu tuwe na utalii wa afya, watu watoke nchi jirani wapate matibabu. Tanzania iwe kituo cha ubingwa wa mambo ya afya kwa nchi tunazopakana nazo,” amesema Rais Samia.

Kuhusu ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Maweni, Rais Samia amesema Serikali yake itapeleka Sh. 2 bilioni, kwa ajili ya kumalizia majengo yaliyobakia ili hospitali hiyo ikamilike.

Aidha, Rais Samia amesema hospitali hiyo inatarajia kuanza kutoa baadhi ya huduma ikiwemo ya vipimo vya CT-Scan, kuanzia Novemba Mosi, mwaka huu.

Amesema upanuzi wa hospitali hiyo utasaidia kusogeza huduma za afya karibu na wananchi, pamoja na kuokoa fedha ambazo ilikuwa inatumia kufuata huduma katika Hospitali nyingine kubwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!