Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Tanzania kujitangaza kibiashara soko la EAC
Habari Mchanganyiko

Tanzania kujitangaza kibiashara soko la EAC

Pindi Chana, Balozi wa Tanzania nchini Kenya
Spread the love

BALOZI wa Tanzania nchini Kenya, Pindi Chana imeiomba sekta binafsi kujitokeza ili kushiriki maadimisho ya biashara hapa nchini yatakayofanyika Aprili 26 mwaka huu kwa lengo la kukuza uchumi wa viwanda. Anaripoti Angel Willium … (endelea).

Maadhimisho hayo yameandaliwa kwa ushirikiano wa wizara ya mambo ya nje nchini Kenya na wizara ya viwanda na biashara hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa Balozi Chana amesema serikali imeandaa maadhimisho ya kibiashara, ili kuzitangaza bidhaa za hapa nchini katika soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

“Soko kubwa kwa EAC lipo nchini hivyo bidhaa zetu tunatakiwa kupeleka katika nchi hiyo ambayo ni majirani zetu, wafanyabiashara wa viwandani na wajasiriamali wanatakiwa kuzitangaza bidhaa mbalimbali kama vitenge, sabuni, maji ya kunywa,dawa za mswaki,” amesema

“Tunatarajia kufanya wiki maalumu ya kuzitangaza bidhaa za Tanzania, ili ziweze kufika nchini ya Kenya hivyo nachukua nafasi hii kuwa karibisha wafanyabiashara wa viwanda na wajasiria mali wajitokeze katika siku hivyo,”amesma chana.

Aidha, Mkurugenzi wa kampuni ya Lake Group, Khaled Hassani amesema, Kenya ni nchi ambayo ina biashara nyingi na wanahakikisha wanazuia biashara yoyote kutoka nje kuingia nchini mwao.

Amesema kampuni yake ilikutana na vipingamizi vingi ilipotaka kuingia nchini Kenya na kwamba kwa sasa wanashika nafasi ya pili mauzo ya gesi.

Maadhimisho yatakuwa yanafanyika kila mwaka katika sikukuu ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

error: Content is protected !!