Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Tanzania inavyotatua matatizo ya wakimbizi
Habari Mchanganyiko

Tanzania inavyotatua matatizo ya wakimbizi

Khamis Chilo, Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imesema, jitihada zinaendelea kufanyika ili kumaliza tatizo la wakimbizi nchini humo kwa kuwarejesha makwao kwa kushirikiana na Jumuiya za Kimataifa na nchi wanazotoka. Anaripoti Jemima Samwel, DMC…(endelea).

Mara baada ya wakimbizi hao kuondoka, maeneo yote ya kambi za wakimbizi yatarejeshwa serikalini ili mamlaka zinazohusika ziweze kuyapangia matumizi stahiki.

Hayo yamesemwa leo Jumanne, tarehe 27 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Khamis Chilo wakatio akijibu swali la Agustine Holle, Mbunge wa Kasulu Vijijini (CCM).

“Kumekuwa na mgogoro wa ardhi wa muda mrefu baina ya kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu na Kata ya Makere, je ni lini Serikali itatatua mgogoro huo,” ameuliza Holle

Akijibu swali hilo, naibu waziri wa wizara hiyo, Chilo amesema, kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu ilianzishwa mwaka 1996, kwa ajili ya kupokea wakimbizi kutoka nchi ya DRC.

Amesema, wakati wa uanzishwaji wa kambi hiyo, hakukuwa na mgogoro wa ardhi kwa sababu, lilikuwa eneo lisilotumika aidha pamoja na eneo la kambi, Serikali lilitenga eneo lingine la akiba kwa ajili ya wakimbizi iwapo eneo la awali litazidiwa.

“Kadri muda unavyokwenda, wananchi walianza kuvamia eneo la akiba kwa lengo la kuwatumia wakimbizi kama vibarua katika shughuli za kilimo katika eneo hilo.”

“Kwa kuzingatia maelezo hayo, ni wazi hakuna mgogoro wa ardhi baina ya kambi ya Nyarugusu na kata ya Makere, bali ni suala la uelewa ambapo wananchi wanaendelea kuelimishwa juu ya matumizi ya eneo hilo,” amesema Chilo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!