Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Takukuru yavimbia wakandarasi, ‘yarejesha’ mil 420 Tanesco
Habari Mchanganyiko

Takukuru yavimbia wakandarasi, ‘yarejesha’ mil 420 Tanesco

Brigedia Jenerali, John Mbungo, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru
Spread the love

 

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), imerejesha vifaa ghafi vya umeme vyenye thamani ya zaidi Sh. 420 milioni kwa Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (Tanesco). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Vifaa hivyo vilivyokuwa vikishikiliwa na wakandarasi wanne, ambapo waliokuwa wakitekeleza Awamu ya Pili ya Mradi wa Umeme Vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Mawakala hao ni Derm Electrics (T) Ltd, M/S JV States Grid Electrical & Technical Works Ltd. Nakuroi Investments na Urban and Rural Engineering Services Ltd.

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 27 Februari 2021, na Mkurugenzi Mkuu Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo wakati akikabidhi vifaa hivyo kwa Naibu Mkurugenzi Tanesco, Mhandisi  Isaack Chanji, kwenye ofisi za shirika hilo, Tawi la Mikocheni, jijini Dar es Salaam.

Brigedia Mbungo amesema, vifaa hivyo vimerudishwa baada ya agizo lake alilolitoa mkoani Iringa mwishoni mwa 2020, lililowataka wakandarasi waliokuwa wakidaiwa na serikali vifaa, kuvirejesha ndani ya siku 14.

“Katika kutekeleza agizo hili, baadhi ya Wakandarasi walifika katika ofisi za Takukuru kuhakiki na kutambua aina na idadi ya vifaa ghafi vya umeme wanavyotakiwa kuvirejesha TANESCO,” amesema Brigedia Mbungo.

Vifaa vilivyorejeshwa Tanesco na Takukuru ni mashine za usambazaji umeme (Transfoma) 30 zenye ukubwa tofauti tofauti pamoja na taa za umeme za matumizi madogo ya umeme (Energy Saver Bulbs) 20,000.

Mkuu huyo wa Takukuru amesema taasisi hiyo iliamua kuingilia kati sakata hilo, kwa kuwa wakandarasi hao walipaswa kuvirudisha tangu 2017.

“Vifaa hivi vilitakiwa viwe vimerejeshwa TANESCO  2017 na Mkandarasi M/S JV States Grid Electrical & Technical Works Ltd, ambaye alitekeleza Mradi wa REA II Mkoani Kigoma na kuukamilisha tangu mwaka 2017,” amesema Brigedia .

Aidha, Brigedia Mbungo amesema kuna baadhi ya wakandarasi wamewasilisha taarifa zao za miradi  Takukuru, kwa ajili ya kuhakikiwa ili warudishe vifaa ghafi.

“Vilevile, wapo baadhi ya Wakandarasi ambao tayari wamewasilisha taarifa zao za miradi ili zihakikiwe na TAKUKURU tayari kwa kuanza zoezi la kurejesha vifaa ghafi,” amesema Brigedia Mbungo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!