Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Takukuru yamshikilia Mfanyabiashara Dodoma
Habari za Siasa

Takukuru yamshikilia Mfanyabiashara Dodoma

Brigedia Jenerali, John Mbungo
Spread the love

TAALIB Karim Mbowe, mfanyabiashara na mmiliki wa Kampuni ya White Star Investiment jijini Dodoma anashikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa tuhuma tatu ikiwemo kukwepa kodi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma …(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa ya Takukuru leo tarehe 16 Agosti 2020, Mbowe anatuhumiwa kukwepa kulipa kodi, udanyanyifu na utakatishaji fedha haramu.

Mbowe kupitia kampuni hiyo, ni wafanyabiashara ya usafirishaji ndani nan je ya nchi kwa kutumia malori.

Kwenye taarifa hiyo iliyosainiwa na Doreen Kapwani, Ofisa Uhusiano wa Takukuru kwa niaba ya Brigedia Jenerali John Mbungo, Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Takukuru inaendelea kuchunguza umiliki wa vichwa vya malori (Treller) zaidi ya 100 vinazomilikiwa na mfanyabiashara huyo.

Taasisi hiyo pia inachunguza mikopo yake ya Dola za Marekani zaidi ya 3,000,000 kutoka Benki ya Barclays na dola 540,000 kutoka katika Benki ya Equity.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!