Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Takukuru watakiwa kutoa ruhusa Sethi kuhojiwa
Habari Mchanganyiko

Takukuru watakiwa kutoa ruhusa Sethi kuhojiwa

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeombwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuamuru mtuhumiwa wa kesi ya uhujumu uchumi, Harbinder Sethi kuchukuliwa gerezani kwa ajili ya kuhojiwa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Sethi na James Rugemarila wanasota rumande kutokana na kukabiliwa na mashtaka 12 ya utakatishaji fedha na uhujumu uchumi kwa kula njama, kughushi na kutoa nyaraka za kughushi, kujihusisha na mtandao wa uhalifu pamoja na kuisababishia serikali hasara.

Wakili wa TAKUKURU, Leonard Swali ametoa ombi hilo leo tarehe 25 Oktoba 2018 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, akisema kuwa wachunguzi wa taasisi hiyo watamchukua Sethi gerezani ili kumhoji kwa ajili ya kukamilisha uchunguzi.

Baada ya ombi hilo, Hakimu Shaidi ali ihairisha kesi hiyo hadi tarehe 8 Novemba 2018 baada ya mawakili wa pande zote mbili kuafikiana kuhusu mahojiano hayo, ambapo Wakili upande wa utetezi, Dorah Mallaba aliieleza Mahakama hiyo kwamba, wakati mteja wake Sethi anachukuliwa maelezo, mawakili wake wawepo.

Tarehe 8 Novemba 2018, kesi hiyo inatarajiwa kutajwa pamoja na kuangalia iwapo uchunguzi wake utakuwa umekamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!