TIMU ya Taifa Tanzania ‘Taifa Stars’ imezinduka usingizi baada ya kuitandika DR Congo kwa mabao 2-0 katika mchezo wa kirafiki wa Kimataifa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Huu ni mchezo wa pili wa kirafiki Taifa Stars kucheza baada ya wiki iliyopita kukubali kipigo dhidi ya Algeria cha mabao 4-1 uliochezwa ugenini.
Bao la kwanza kwa Taifa Stars lilipachikwa kwa kichwa na nahodha wa timu hiyo Mbwana Samatta katika dakika ya 74 ya mchezo kabla ya Shiza Kichuya kupachika bao la pili dakika ya 87.
Ushindi huo utaisaidia Taifa Stars kuweza kupanda katika viwango vya ubora wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) kutokana na kushinda dhidi ya timu iliyokuwa juu kwa viwango zaidi yao.
DR Congo inashika nafasi ya tatu kwa ubora katika viwango vya Shirikisho la Mpira wa Miguu Africa (CAF) huku ikiwa nafasi ya 39 Fifa wakati Tanzania ipo nafasi ya 149 duniani na 46 Afrika.
Leave a comment