Thursday , 18 April 2024
Home Kitengo Michezo Taifa Stars kutupa karata muhimu kuelekea Kombe la Dunia 2022
Michezo

Taifa Stars kutupa karata muhimu kuelekea Kombe la Dunia 2022

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kikiwa mazoezini
Spread the love

TIMU ya soka ya Tanzania “Taifa Stars” inashuka katika dimba lake la nyumbani la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam kuwakabili DR Congo, kuwania kufuzu Kombe la Dunia Qatar 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Ni leo Alhamisi, tarehe 11 Novemba 2021 kuanzia saa 10:00 jioni.

Stars inayoongoza kundi J ikiwa na pointi saba sawa na Benin lakini ikiwa na uwiano mzuri wa magoli ya kufungwa na kufunga, itashuka tena dimba hilohilo, tarehe 14 Novemba 2021, kuwakabili Madagascar.

Katika kundi hilo, Congo inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi tano huku Madagascar ikishika mkia ikiwa na pointi tatu.

Mchezo mwingine wa kundi hilo, utapigwa leo kuanzia saa 1:00 usiku, Benin itakapowakalibisha Madagascar.

Aidha, Serikali ya Tanzania chini ya Waziri Mkuu wake, Kassim Majaliwa kwa nyakati tofauti aliitembelea Stars kwenye uwanja wa mazoezi na kambini na kuzungumza nao.

Majaliwa alikutana na wadau wa soka nchini humo na kuchangisha Sh.1.6 bilioni ili kutoa hamasa kwa kambi hiyo katika michezo yote ili kuhakikisha inafuzu michuano hiyo mikubwa ya dunia itakayopigwa Qatar mwakani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!