Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Taifa Stars kutua Cape Verde na Dreamliner
Michezo

Taifa Stars kutua Cape Verde na Dreamliner

ATCL Dreamliner
Spread the love

TIMU ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars itatua jijini Praia, nchini Cape verde na Dreamliner mali ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kuvaana na wenyeji hao kwenye mchezo wa kutafuta tiketi ya kufuvu kwenye fainali za kombe la matifa huru ya Afrika (AFCON) unaotarajia kuchezwa 12 Octoba 2018. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Akiongea mbele ya waandishi wa habari leo Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe alisema ndege ya hiyo ambayo itabeba wachezaji pamoja na mashabiki 200 itarejea nchini mara baada ya mchezo huo kumalizika ili kuwahi kujiandaa na mchezo wa marudiano utakaochezwa 16 Octoba, 2018 jijini Dar es Salaam.

“Kitendo cha timu kushuka Cape Verde na Dreamliner, tena ndege ya nyumbani, tayari tumekwishawapiga goli mbili, hizo goli nyingine namuachia Amunike na benchi la ufundi waongezee,” amesema Waziri Mwakyembe.

Waziri huyo aliongezea kuwa kutokana na ndege hiyo kuchukua watu 200 huku wakati msafara mzima wa Taifa Stars utakuwa na watu 31, hivyo kutakuwa na nafasi kwa mashabiki watakaopenda kusafiri na timu hiyo itawalazimu kuchangia dola za kimarekani 1,500 sawa na S. 3.5 milioni kwa tiketi ya kwenda na kurudi.

“Wachezaji na viongozi watakaokwenda Cape Verde hawatazidi 31, Dreamliner ina uwezo wa kuchukua watu zaidi ya 200, hivyo tunaomba mashabiki wajitahidi kununua tiketi tukaishabikie timu yetu ya taifa,”

Stars watakuwa wagenini kwenye mchezo huo wa kundi L, ambalo linajumuisha timu za Uganda ambaye ndio kinara wa kundi hili akifuatiwa na Cape Verde wanashika nafasi ya pili huku Tanzania ikiwa nafasi ya tatu ikiwa na alama mbili na Lesotho akiburuza mkia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!