Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Taifa Stars kuingia kambini leo, kuivutia kasi Guinea
Michezo

Taifa Stars kuingia kambini leo, kuivutia kasi Guinea

Kim Poulsen Kocha wa Taifa Stars
Spread the love

 

TIMU ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaingia kambini hii leo kwa ajili ya kujiandaa na michezo miwili ya kirafikia pamoja na mchezo wa kufuzu kwa michuano ya kombe la mataifa Afrika (AFCON) dhidi ya Equatorial Guinea. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Wachezaji walioitwa wataanza kuingia kambini hii leo jioni kwenye hotel ya Tiffany Diamond iliyopo jijini Dar es Salaam.

Kocha mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen aliita wachezaji 43, ambao watasafiri kuelekea nchini Kenya kwa ajili ya kucheza michezo miwili ya kirafiki tarehe 16 na 18 Machi 2021, na kisha tarehe 19 kikosi hiko kitasafiri kueleke Guinea kwa ajili ya mchezo wa kufuzu AFCON.

Mchezo huo dhidi ya Equatorial Guinea utapigwa siku ya tarehe 25 Machi, 2021.

Taifa Stars ipo Kundi J inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi nne, huku ikiwa imebakisha michezo miwili ambayo inahitaji ushindi ili iweze kufuzu.

Vinara wa kundi hilo mpaka sasa ni Tunisia akiwa na pointi 10, ikifuatiwa na Equatorial Guinea kwenye nafasi ya pili wakiwa na pointi sita, nafasi ya tatu Taifa Stars ikiwa na pointi nne, huku Libya ikiwa mkiani wakiwa na pointi tatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!