Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Taasisi za dini zaibua dosari uchaguzi 2020, Samia ajibu
Habari Mchanganyiko

Taasisi za dini zaibua dosari uchaguzi 2020, Samia ajibu

Spread the love
JUMUIYA ya Kikristo Tanzania (CCT), imesema taasisi za dini hazikushirikishwa katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa 2020, baada ya kukosa vibali, tofauti na chaguzi zilizopita.Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro…(endelea).
Kauli hiyo imetolewa leo Alhamisi, tarehe 8 Julai 2021 na Mwenyekiti wa CCT, Askofu  Alinikisya Cheyo, mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano mkuu wa jumuiya hiyo uliofanyika mkoani Morogoro.
Askofu Cheyo ameiomba Serikali ya Rais Samia, izishirikishe taasisi hizo katika michakato ya uchaguzi, kama ilivyokuwa hapo awali.
“Ushirki wa taaisi za dini  katika Uchaguzi Mkuu wa 2020 haukuwepo kabisa, mara baada ya kukosa kibali katika mamlaka husika. Tunaomba kama tulivyokuwa tunaendelea huko nyuma, tushirikishwe zaidi,” amesema Askofu Cheyo.
Mbali na malalamiko hayo, Askofu Cheyo amesema taasisi hizo zinaomba zishirikishwe katika michakato ya kidemokrasia, hasa kwenye masuala ya utoaji elimu ya uraia na uangalizi wa uchaguzi, kwa wananchi.
“Tunaleta kwako ombi la taasisi za dini kuhusishwa kikamilifu katika michakato ya kidemokrasia hasa katika  kuwafundisha wananchi  mambo ya uraia na uangalizi wa uchaguzi mbalimbali,” amesema Askofu Cheyo.
Mwenyekiti huyo wa CCT, amesema taasisi za dini zina mchango mkubwa katika masuala ya utungwaji na marekebisho ya  sheria, hivyo zinapaswa kushirikishwa.
“Pendelezo letu la kwanza, ni nafasi ya taasisi za kidini kuhusishwa katika michakato ya kidemokrasia, taasisi zimekuwa zikishiriki kikamilifu katika michakato ya kidemokrasia,  kutokana na ukaribu na muundo wake,” amesema Askofu Cheyo na kuongeza:
“Ikiwa pamoja  na kutoa maoni katika utungwaji na maboresho ya sheria, kutoa elimu ya uraia na kushiriki uchaguzi.”
Akijibu ombi la taasisi hizo kushirikishwa katika michakato ya uchaguzi, Rais Samia amesema Serikali yake itafuatilia masuala ya kisheria,  ili kuona namna taasisi hizo zinashiriki.
 “Kuna taasisi zinashiriki mambo ya uchaguzi zilizosajiliwa chini ya Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ( NGO’s), nadhani hapa kuna utata wa kisheria hizi zimesajiliwa huku na zingine kule.  Kwa maombi yenu haya inabidi tuangalie sheria zetu zinasemaje,  ili kuwapa uhalali wa kufanya shughuli hizo,” amesema Rais Samia.
Kuhusu taasisi hizo kushiriki katika utungwaji na maboresho ya sheria, Rais Samia amesema kabla ya Bunge kupitisha sheria,  hutoa nafasi kwa wananchi kutoa maoni yao kuhusu mchakato husika, hivyo amezitaka zitumie nafasi hiyo.
“Niseme kwamba katika kutoa maoni kwenye maboresho na utungaji Sheria, Bunge limetoa siku maalumu kutoa maoni kwa wananchi. Siku hii taasisi zinaweza kushiriki kutoa maoni yao.  Hili la kushirikishwa kutoa elimu ya uraia nalo ni zuri sana, tutawashirikisha,” amesema Rais Samia.
Hata hivyo, Rais Samia amesema Serikali zilizopita zilikuwa zinashirikisha taasisi za dini,  katika masuala ya kidemokrasia na kukumbushia namna viongozi wa dini walivyoshiriki katika Bunge la Katiba.
“Serikali zilizopita zimekuwa zikifanya hivyo, kushirikisha viongozi ikiwemo katika masuala ya kidemokrasia. Nakumbuka nilipokuwa makamu mwenyekiti wa  Bunge la Katiba,  sura za baadhi ya viongozi wa dini niliziona,” amesema Rais Samia na kuongeza:
“ Huku ni kushirikishwa katika mambo ya kidemokrasia , nitafuata nyayo za walionitangulia kufuata hili.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!