Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Sumaye – sasa tunaelekea vijijini
Habari za Siasa

Sumaye – sasa tunaelekea vijijini

Frederick Sumaye, Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania
Spread the love

MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Pwani, Fredrick Sumaye, amesema chama chake kitazunguka nchi nzima kuelimisha wananchi juu ya haki zao, anaandika Catherine Kayombo.

Amesema elimu hiyo itatolewa katika vijiji na vitongoji vyote nchini, ili wananchi waweze kujua haki zao, ili kuweza kuamka na kupinga demokrasia kandamizi inayoota mizizi.

Hakutaja tarehe ya kuanza mpango huo, lakini alisema kuwa hadi mwisho wa mwaka kesho nchi nzima itakuwa imeelimishwa kuhusu haki za raia.

Sumaye amesema hayo leo katika ofisi za kanda, Magomeni, Dar es Salaam, alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari kuhusu kile alichoita “mambo yanatotuhusu sote kwa maslahi ya taifa.”

Alizungumzia nafasi ya demokrasia ya vyama vingi vya siasa, mfumo wa demokrasia kandamizi, utawala wa demokrasia sahihi ya vyama vingi, utawala bora na demokrasia kandamizi, na kazi ya vyama vya upinzani.

“Watu wanadhani udikteta ni lazima uingie madarakani kwa mabavu. Hapana! Unaweza kuwa dikteta hata kama umeningia madarakani kwa kura, mradi mfumo uliotumia ni demokrasia pingamizi,” alisema.

Moja ya haki za msingi ambayo Sumaye alizungumzia ni haki ya kutoa na kupata habari, ambayo pia inalindwa na ibara ya 18 ya katiba ya nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!