Saturday , 10 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Sumatra waingia kwenye shutuma nzito
Habari Mchanganyiko

Sumatra waingia kwenye shutuma nzito

Mitumbwi ya wavuvi katika Ziwa Tanganyika
Spread the love

MBUNGE wa Buyungu, Mwalimu, Bilago Kasuku (Chadema) ameibana serikali na kuitaka ieleze ni kifungo gani cha sheria kinaipaMamlaka ya Usimamizi wa Usafiri wa Ardhini na Majini (Sumatra) kutoza ushuru kwa wavuvi na wakati huo huo haifanyi hivyo kwa matrekta ya kilimo, anaandika Dany Tibason.

“Je, Serikali haioni kuwa inadidimiza wavuvi kwa kuwarundikia tozo nyingi na kuwafanya waendelee kuwa Maskini?’’ amehoji Kasuku.

Mwalimu Bilago alitoa kauli hiyo leo bungeni alipokuwa akiuliza swali na nyongeza kwa kuitaka serikali ieleze kama Sumatra kufanya hivyo siyo kudidimiza juhudi za wavuvi.

Akiuliza swali la msingi kwa niaba ya mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT Wazalendo) amehoji kuhusina na Sumatra kutoa vibali vya usafiri kwa wavuvi wa Ziwa Tanganyika.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani amesema Sumatra hatoi vibali wala haitozi ushuru kwa vyombo vya usafiri majini nchini ikiwa ni pamoja na wavuvi wa Ziwa Tanganyika.

Ngonyani amesema Sumatra inalo jukumu la kukagua ubora wa vyombo vya usafiri majini ikiwa ni pamoja na vya uvuvi na kutoa cheti cha ubora.

“Moja ya majukumu ya msingi ya Sumatra katika vyombo vya usafiri na vya uvuni ni kuhakikisha vyombo hivyo ni salama kabla ya kuanza kufanya shughuli za majini,’’ amesema.

Amesema mamlaka hiyo inapokagua vyombo vya usafiri majini kwa mujibu wa sehemu ya 11 kanuni ya 9 ya kanuni za sheria ambapo wenye vyombo vya usafiri ikiwa ni pamoja na vya uvuvi.

Kutokana na hali hiyo, Ngonyani amesema serikali haikusudii kudidimiza wavuvi wala haijawarundikia tozo nyingi ambazo ambazo zitawafanya wawe maskini bali inawahakikishia mazingira salama kwa ajili ya kufanya shighuli zao za uvuvi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!