Friday , 9 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Sumatra kutoa leseni ya muda mfupi
Habari Mchanganyiko

Sumatra kutoa leseni ya muda mfupi

Spread the love

MAMLAKA YA Udhibiti na Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imefungua dirisha la maombi ya leseni za muda mfupi kwa wamiliki wa mabasi yenye uwezo wa kubeba abiria 50, yanayotaka kwenda mikoa yenye uhitaji mkubwa katika kipindi cha sikukuu za mwisho wa mwaka. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa iliyotolewa hivi karibuni na SUMATRA inaeleza kuwa, ili mabasi hayo yapewe leseni hizo, yanatakiwa kufungwa mfumo wa kufuatilia mwenendo wa mabasi (VTS) na masharti mengine ya uombaji leseni yatazingatiwa.

Katika sharti lingine, wamiliki wa mabasi wanatakiwa kuuza tiketi kwa njia ya kielektroniki itakayowezesha abiria kukata tiketi kwa urahisi.

Katika hatua nyingine, SUMATRA imewataka abiria wanaotarajia kusafiri nyakati za sikukuu kukata tiketi zao mapema, pamoja na kutafuta taarifa sahihi za kiwango cha nauli kutoka katika mamlaka hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!